Thursday, 13 October 2011

Nyama ya Kukaanga

Viungo:
  1. Nyama
  2. Kitunguu
  3. Dhania
  4. Pilipili hoho
  5. Nyanya
  6. Chumvi
  7. Mafuta ya maji
Kuandaa:
  1. Kata nyama vipande vidogo kisha chemsha hadi iive.
  2. Weka mafuta ya maji kwa sufuria.
  3. Weka kitunguu na ukaange hadi iwe na rangi ya kahawia.
  4. Ongeza nyanya, dhania na pilipili hoho kisha kaanga hadi iive.
  5. Ongeza nyama iliyochemshwa kisha pika kwa moto wa chini hadi viungo vyote vichanganyikane.
 Pakua na wali au ugali

2 comments:

  1. asanti kwa kitoweo loe nimepata chakula cha kupika for a change from the common ugali na sukuma ama nyama boil

    ReplyDelete
  2. Karibu...brace yourself! Samaki wa mchuzi on the way.

    ReplyDelete