Thursday, 12 April 2012

Samaki wa Kukaanga

Viungo:
  1. Samaki au minofu ya samaki
  2. Maji ya limau au ndimu
  3. Chumvi
  4. Kitunguu Saumu
  5. Mafuta ya maji

Kuandaa:
  1. Weka samaki au minofu ya samaki, maji ya limau au ndimu, kitunguu saumu, chumvi kwa bakuli kubwa na uweke kando kwa dakika 20-30.
  2. Weka mafuta ya maji kwa karai kwa moto wa chini.
  3. Toa samaki au minofu ya samaki kwa bakuli ulio na mchanyiko wa maji ya limau au ndimu kisha uweke kwa karai ya mafuta na upike hadi igeuke kuwa rangi ya udhurungi kila upande.
  4. Ikiisha iva epua. 
Pakua na sukuma wiki.

No comments:

Post a Comment