Thursday, 12 April 2012

Kuku wa Kupaka

Viungo:
  1. Minofu ya kuku
  2. Vitunguu
  3. Pilipili
  4. Tangawizi mbichi
  5. Mafuta ya maji
  6. Curry Poda
  7. Chumvi
  8. Nyanya
  9. Kitunguu Saumu
  10. Maji ya nazi
Kuandaa
  1. Weka vitunguu, pilipili, tangawizi mbichi na kitunguu saumu kwa kinu na uponde hadi viungo viwe laini.
  2. Ongeza maji. Weka mafuta ya maji kwa sufuria kwa moto wa chini.
  3. Ongeza mchanganyiko wa viuongo ulivyoponda kwa kinu na changanya hadi ziive kwa mda wa dakika 5 hadi 8.
  4. Ongeza nyanya na upike kwa mda wa dakika 3 hadi 4. Kisha ongeza kuku, chumvi, pilipili na maji ya nazi.
  5. Punguza moto na uwache kuku iive kwa mda wa dakika 30.
  6. Ongeza maji.
  7. Ikishaiva epua
Pakua na chapati.


No comments:

Post a Comment