Wednesday, 19 October 2011

Mchuzi wa Kuku (Kienyeji)

Viungo:
  1. Minofu ya Kuku wa kienyeji
  2. Nyanya mbili kubwa
  3. Kitunguu kimoja kikubwa
  4. Chumvi
  5. Mafuta ya maji
  6. Kitunguu Saumu
  7. Dhania
  8. Pili pili hoho
Kuandaa:
  1. Chemsha kwa mda wa lisaa limoja (Kuku wa kienyeji huwa wagumu na hitaji mda zaidi kufanya walainike).
  2. Ikishalainika na mchuzi umebaki, toa mchuzi na uweke kando.
  3. Kaanga kitunguu kwa mafuta maji hadi kiwe na rangi ya kahawia.
  4. Ongeza kitunguu saumu na chumvi na ukoroge hadi viungo vyote vichanganyikane.
  5. Ongeza nyanya, pili pili hoho na dhania na uongeze kukoroga hadi viungo vyote vichanganyikane.
  6. Ongeza kuku iliyochemshwa na upike kwa dakika kumi hivi.
  7. Ongeza mchuzi uliyoweka kando na uwache iive kwa dakika tano hivi.
Pakua na wali au ugali.

No comments:

Post a Comment